Ayu. 32:18-22 Swahili Union Version (SUV)

18. Kwa kuwa nimejaa maneno;Roho iliyo ndani yangu hunihimiza.

19. Tazama, tumbo langu ni kama divai iliyozibwa;Kama viriba vipya li karibu na kupasuka.

20. Nitanena, ili nipate kutulia;Nitafunua midomo yangu na kujibu.

21. Tafadhali, nisiupendelee uso wa mtu;Wala sitajipendekeza kwa mtu ye yote.

22. Kwani mimi sijui kujipendekeza;Au Muumba wangu angeniondoa kwa upesi.

Ayu. 32