9. Kama moyo wangu ulishawishwa kwa mwanamke,Nami nimeotea mlangoni pa jirani yangu;
10. Ndipo hapo mke wangu na asage kwa mwingine,Na wengine na wainame juu yake.
11. Kwani hilo lingekuwa kosa kuu;Naam, lingekuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi;
12. Kwa kuwa ni moto uteketezao hata Uharibifu,Nao ungeyang’oa maongeo yangu yote.
13. Kama nimeidharau daawa ya mtumishi wangu, au ya kijakazi changu,Waliposhindana nami;
14. Basi Mungu atakapoinuka nitafanya nini?Naye atakapozuru, nitamjibuje?