8. Basi na nipande, mwingine ale;Naam, mazao ya shamba langu na yang’olewe.
9. Kama moyo wangu ulishawishwa kwa mwanamke,Nami nimeotea mlangoni pa jirani yangu;
10. Ndipo hapo mke wangu na asage kwa mwingine,Na wengine na wainame juu yake.
11. Kwani hilo lingekuwa kosa kuu;Naam, lingekuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi;
12. Kwa kuwa ni moto uteketezao hata Uharibifu,Nao ungeyang’oa maongeo yangu yote.
13. Kama nimeidharau daawa ya mtumishi wangu, au ya kijakazi changu,Waliposhindana nami;
14. Basi Mungu atakapoinuka nitafanya nini?Naye atakapozuru, nitamjibuje?
15. Je! Huyo aliyenifanya mimi ndani ya tumbo, siye aliyemfanya na yeye?Si yeye mmoja aliyetufinyanga tumboni?
16. Ikiwa nimewanyima maskini haja zao,Au kama nimeyatia kiwi macho ya mwanamke mjane;
17. Au kama nimekula tonge langu peke yangu,Mayatima wasipate kulila;
18. (La, tangu ujana wangu alikua pamoja nami kama kwa baba;Nami nimekuwa ni kiongozi cha mjane tangu tumbo la mamangu);