Ayu. 31:5-14 Swahili Union Version (SUV)

5. Kwamba nimetembea katika ubatili,Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu;

6. (Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa,Ili Mungu aujue uelekevu wangu);

7. Kwamba hatua yangu imekengeuka na kuiacha njia,Na moyo wangu kuyaandama macho yangu,Tena kwamba kipaku cho chote kimeshikamana na mikono yangu;

8. Basi na nipande, mwingine ale;Naam, mazao ya shamba langu na yang’olewe.

9. Kama moyo wangu ulishawishwa kwa mwanamke,Nami nimeotea mlangoni pa jirani yangu;

10. Ndipo hapo mke wangu na asage kwa mwingine,Na wengine na wainame juu yake.

11. Kwani hilo lingekuwa kosa kuu;Naam, lingekuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi;

12. Kwa kuwa ni moto uteketezao hata Uharibifu,Nao ungeyang’oa maongeo yangu yote.

13. Kama nimeidharau daawa ya mtumishi wangu, au ya kijakazi changu,Waliposhindana nami;

14. Basi Mungu atakapoinuka nitafanya nini?Naye atakapozuru, nitamjibuje?

Ayu. 31