33. Ikiwa kama mwanadamu nimeyafunika makosa yangu,Kwa kuuficha uovu wangu kifuani mwangu;
34. Kwa sababu niliwaogopa mkutano mkubwa,Na dharau la jamaa lilinitia hofu,Hata nilinyamaa kimya, nisitoke mlangoni-
35. Laiti ningekuwa na mtu wa kunisikia!(Tazama, sahihi yangu ni hii, Mwenyezi na anijibu);Laiti ningekuwa na hayo mashitaka yaliyoandikwa na adui yangu!
36. Hakika ningeyachukua mabegani;Ningejifungia mfano wa kilemba.
37. Ningemwambia hesabu ya hatua zanguNingemkaribia kama vile mkuu.
38. Kama nchi yangu yalia juu yangu,Na matuta yake hulia pamoja;
39. Kama nimeyala matunda yake pasipo kulipa,Au kama nimewafanya wenyewe kupotewa na uhai;
40. Miiba na imee badala ya ngano,Na magugu badala ya shayiri.Maneno ya Ayubu yamekoma hapa.