3. Je! Siyo msiba kwa wasio haki,Na hasara kwao watendao uovu?
4. Je! Yeye hazioni njia zangu,Na kuzihesabu hatua zangu zote?
5. Kwamba nimetembea katika ubatili,Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu;
6. (Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa,Ili Mungu aujue uelekevu wangu);
7. Kwamba hatua yangu imekengeuka na kuiacha njia,Na moyo wangu kuyaandama macho yangu,Tena kwamba kipaku cho chote kimeshikamana na mikono yangu;
8. Basi na nipande, mwingine ale;Naam, mazao ya shamba langu na yang’olewe.