Ayu. 31:3-8 Swahili Union Version (SUV)

3. Je! Siyo msiba kwa wasio haki,Na hasara kwao watendao uovu?

4. Je! Yeye hazioni njia zangu,Na kuzihesabu hatua zangu zote?

5. Kwamba nimetembea katika ubatili,Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu;

6. (Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa,Ili Mungu aujue uelekevu wangu);

7. Kwamba hatua yangu imekengeuka na kuiacha njia,Na moyo wangu kuyaandama macho yangu,Tena kwamba kipaku cho chote kimeshikamana na mikono yangu;

8. Basi na nipande, mwingine ale;Naam, mazao ya shamba langu na yang’olewe.

Ayu. 31