28. Hilo nalo lingekuwa uovu wa kuadhibiwa na waamuzi;Kwani ningemwambia uongo Mungu aliye juu.
29. Kama nilifurahi kwa kuangamia kwake huyo aliyenichukia,Au kujitukuza alipopatikana na maovu;
30. (Naam, sikukiacha kinywa changu kufanya dhambiKwa kuutaka uhai wake kwa kuapiza);
31. Kama watu wa hemani mwangu hawakunena,Ni nani awezaye kumpata mtu asiyeshibishwa na yeye kwa nyama?
32. Mgeni hakulala njiani;Lakini nilimfungulia msafiri milango yangu;
33. Ikiwa kama mwanadamu nimeyafunika makosa yangu,Kwa kuuficha uovu wangu kifuani mwangu;
34. Kwa sababu niliwaogopa mkutano mkubwa,Na dharau la jamaa lilinitia hofu,Hata nilinyamaa kimya, nisitoke mlangoni-
35. Laiti ningekuwa na mtu wa kunisikia!(Tazama, sahihi yangu ni hii, Mwenyezi na anijibu);Laiti ningekuwa na hayo mashitaka yaliyoandikwa na adui yangu!
36. Hakika ningeyachukua mabegani;Ningejifungia mfano wa kilemba.
37. Ningemwambia hesabu ya hatua zanguNingemkaribia kama vile mkuu.
38. Kama nchi yangu yalia juu yangu,Na matuta yake hulia pamoja;
39. Kama nimeyala matunda yake pasipo kulipa,Au kama nimewafanya wenyewe kupotewa na uhai;
40. Miiba na imee badala ya ngano,Na magugu badala ya shayiri.Maneno ya Ayubu yamekoma hapa.