25. Kama nilifurahi kwa kuwa mali yangu yalikuwa mengi,Na kwa sababu mkono wangu umepata vitu vingi;
26. Kama nililitazama jua lilipoangaza,Au mwezi ukiendelea katika kung’aa;
27. Na moyo wangu umeshawishwa kwa siri,Na midomo yangu imeubusu mkono wangu;
28. Hilo nalo lingekuwa uovu wa kuadhibiwa na waamuzi;Kwani ningemwambia uongo Mungu aliye juu.
29. Kama nilifurahi kwa kuangamia kwake huyo aliyenichukia,Au kujitukuza alipopatikana na maovu;