23. Kwani msiba utokao kwa Mungu ulikuwa na kitisho kwangu,Na kwa sababu ya ukuu wake sikuweza kufanya neno.
24. Ikiwa nimeifanya dhahabu kuwa tumaini langu,Na kuiambia dhahabu safi, Wewe u tegemeo langu;
25. Kama nilifurahi kwa kuwa mali yangu yalikuwa mengi,Na kwa sababu mkono wangu umepata vitu vingi;
26. Kama nililitazama jua lilipoangaza,Au mwezi ukiendelea katika kung’aa;
27. Na moyo wangu umeshawishwa kwa siri,Na midomo yangu imeubusu mkono wangu;
28. Hilo nalo lingekuwa uovu wa kuadhibiwa na waamuzi;Kwani ningemwambia uongo Mungu aliye juu.
29. Kama nilifurahi kwa kuangamia kwake huyo aliyenichukia,Au kujitukuza alipopatikana na maovu;
30. (Naam, sikukiacha kinywa changu kufanya dhambiKwa kuutaka uhai wake kwa kuapiza);
31. Kama watu wa hemani mwangu hawakunena,Ni nani awezaye kumpata mtu asiyeshibishwa na yeye kwa nyama?
32. Mgeni hakulala njiani;Lakini nilimfungulia msafiri milango yangu;
33. Ikiwa kama mwanadamu nimeyafunika makosa yangu,Kwa kuuficha uovu wangu kifuani mwangu;