Ayu. 31:23-33 Swahili Union Version (SUV)

23. Kwani msiba utokao kwa Mungu ulikuwa na kitisho kwangu,Na kwa sababu ya ukuu wake sikuweza kufanya neno.

24. Ikiwa nimeifanya dhahabu kuwa tumaini langu,Na kuiambia dhahabu safi, Wewe u tegemeo langu;

25. Kama nilifurahi kwa kuwa mali yangu yalikuwa mengi,Na kwa sababu mkono wangu umepata vitu vingi;

26. Kama nililitazama jua lilipoangaza,Au mwezi ukiendelea katika kung’aa;

27. Na moyo wangu umeshawishwa kwa siri,Na midomo yangu imeubusu mkono wangu;

28. Hilo nalo lingekuwa uovu wa kuadhibiwa na waamuzi;Kwani ningemwambia uongo Mungu aliye juu.

29. Kama nilifurahi kwa kuangamia kwake huyo aliyenichukia,Au kujitukuza alipopatikana na maovu;

30. (Naam, sikukiacha kinywa changu kufanya dhambiKwa kuutaka uhai wake kwa kuapiza);

31. Kama watu wa hemani mwangu hawakunena,Ni nani awezaye kumpata mtu asiyeshibishwa na yeye kwa nyama?

32. Mgeni hakulala njiani;Lakini nilimfungulia msafiri milango yangu;

33. Ikiwa kama mwanadamu nimeyafunika makosa yangu,Kwa kuuficha uovu wangu kifuani mwangu;

Ayu. 31