22. Basi bega langu na lianguke kutoka mahali pake,Na mkono wangu uvunjike mfupani mwake.
23. Kwani msiba utokao kwa Mungu ulikuwa na kitisho kwangu,Na kwa sababu ya ukuu wake sikuweza kufanya neno.
24. Ikiwa nimeifanya dhahabu kuwa tumaini langu,Na kuiambia dhahabu safi, Wewe u tegemeo langu;
25. Kama nilifurahi kwa kuwa mali yangu yalikuwa mengi,Na kwa sababu mkono wangu umepata vitu vingi;
26. Kama nililitazama jua lilipoangaza,Au mwezi ukiendelea katika kung’aa;