17. Au kama nimekula tonge langu peke yangu,Mayatima wasipate kulila;
18. (La, tangu ujana wangu alikua pamoja nami kama kwa baba;Nami nimekuwa ni kiongozi cha mjane tangu tumbo la mamangu);
19. Ikiwa nimemwona mtu kuangamia kwa kukosa nguo,Au wahitaji kukosa mavazi;
20. Ikiwa viuno vyake havikunibarikia,Au kama hakupata moto kwa manyoya ya kondoo zangu;
21. Ikiwa nimewainulia mayatima mkono,Nilipoona msaada wangu langoni;