Ayu. 31:17-21 Swahili Union Version (SUV)

17. Au kama nimekula tonge langu peke yangu,Mayatima wasipate kulila;

18. (La, tangu ujana wangu alikua pamoja nami kama kwa baba;Nami nimekuwa ni kiongozi cha mjane tangu tumbo la mamangu);

19. Ikiwa nimemwona mtu kuangamia kwa kukosa nguo,Au wahitaji kukosa mavazi;

20. Ikiwa viuno vyake havikunibarikia,Au kama hakupata moto kwa manyoya ya kondoo zangu;

21. Ikiwa nimewainulia mayatima mkono,Nilipoona msaada wangu langoni;

Ayu. 31