12. Kwa kuwa ni moto uteketezao hata Uharibifu,Nao ungeyang’oa maongeo yangu yote.
13. Kama nimeidharau daawa ya mtumishi wangu, au ya kijakazi changu,Waliposhindana nami;
14. Basi Mungu atakapoinuka nitafanya nini?Naye atakapozuru, nitamjibuje?
15. Je! Huyo aliyenifanya mimi ndani ya tumbo, siye aliyemfanya na yeye?Si yeye mmoja aliyetufinyanga tumboni?
16. Ikiwa nimewanyima maskini haja zao,Au kama nimeyatia kiwi macho ya mwanamke mjane;
17. Au kama nimekula tonge langu peke yangu,Mayatima wasipate kulila;
18. (La, tangu ujana wangu alikua pamoja nami kama kwa baba;Nami nimekuwa ni kiongozi cha mjane tangu tumbo la mamangu);
19. Ikiwa nimemwona mtu kuangamia kwa kukosa nguo,Au wahitaji kukosa mavazi;
20. Ikiwa viuno vyake havikunibarikia,Au kama hakupata moto kwa manyoya ya kondoo zangu;
21. Ikiwa nimewainulia mayatima mkono,Nilipoona msaada wangu langoni;
22. Basi bega langu na lianguke kutoka mahali pake,Na mkono wangu uvunjike mfupani mwake.
23. Kwani msiba utokao kwa Mungu ulikuwa na kitisho kwangu,Na kwa sababu ya ukuu wake sikuweza kufanya neno.
24. Ikiwa nimeifanya dhahabu kuwa tumaini langu,Na kuiambia dhahabu safi, Wewe u tegemeo langu;
25. Kama nilifurahi kwa kuwa mali yangu yalikuwa mengi,Na kwa sababu mkono wangu umepata vitu vingi;
26. Kama nililitazama jua lilipoangaza,Au mwezi ukiendelea katika kung’aa;
27. Na moyo wangu umeshawishwa kwa siri,Na midomo yangu imeubusu mkono wangu;