1. Nilifanya agano na macho yangu;Basi nawezaje kumwangalia msichana?
2. Kwani sehemu ya Mungu itokayo juu ingekuwa nini,Na urithi wa Mwenyezi utokao juu?
3. Je! Siyo msiba kwa wasio haki,Na hasara kwao watendao uovu?
4. Je! Yeye hazioni njia zangu,Na kuzihesabu hatua zangu zote?
5. Kwamba nimetembea katika ubatili,Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu;
6. (Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa,Ili Mungu aujue uelekevu wangu);
7. Kwamba hatua yangu imekengeuka na kuiacha njia,Na moyo wangu kuyaandama macho yangu,Tena kwamba kipaku cho chote kimeshikamana na mikono yangu;