Ayu. 30:4-18 Swahili Union Version (SUV)

4. Hung’oa mboga ya chumvi kwenye kichaka;Na mizizi ya mretemu ni chakula chao.

5. Hufukuzwa watoke kati ya watu;Huwapigia kelele kama kumpigia mwivi.

6. Lazima hukaa katika mianya ya mabonde,Katika mashimo ya nchi na ya majabali.

7. Hulia kama punda vichakani;Hukusanyika chini ya upupu.

8. Wao ni wana wa wapumbavu, naam, watoto wa wahuni;Walifukuzwa kwa mijeledi watoke katika nchi.

9. Na sasa mimi nimekuwa wimbo wao,Naam, nimekuwa simo kwao.

10. Wao hunichukia, na kujitenga nami,Hawaachi kunitemea mate usoni.

11. Kwani ameilegeza kamba yake, na kunitesa,Wala hawajizuii tena mbele yangu.

12. Kwa mkono wangu wa kuume huinuka kundi;Huisukuma miguu yangu kando,Na kunipandishia njia zao za uharibifu.

13. Waiharibu njia yangu,Wauzidisha msiba wangu,Watu wasio na msaidizi.

14. Wanijilia kama wapitao katika ufa mpana;Katikati ya magofu wanishambulia.

15. Vitisho vimenigeukia;Huifukuza heshima yangu kama upepo;Na kufanikiwa kwangu kumepita kama wingu.

16. Sasa nafsi yangu inamwagika ndani yangu;Siku za mateso zimenishika.

17. Wakati wa usiku mifupa yangu huchomeka ndani yangu,Na maumivu yanayonitafuna hayapumziki.

18. Kwa ugonjwa wangu kuwa na nguvu nyingiMavazi yangu yameharibika;Hunikaza kama shingo ya kanzu yangu.

Ayu. 30