Ayu. 30:3-8 Swahili Union Version (SUV)

3. Wamekonda kwa uhitaji na njaa;Huguguna nchi kavu, penye giza la ukiwa na uharibifu.

4. Hung’oa mboga ya chumvi kwenye kichaka;Na mizizi ya mretemu ni chakula chao.

5. Hufukuzwa watoke kati ya watu;Huwapigia kelele kama kumpigia mwivi.

6. Lazima hukaa katika mianya ya mabonde,Katika mashimo ya nchi na ya majabali.

7. Hulia kama punda vichakani;Hukusanyika chini ya upupu.

8. Wao ni wana wa wapumbavu, naam, watoto wa wahuni;Walifukuzwa kwa mijeledi watoke katika nchi.

Ayu. 30