3. Wamekonda kwa uhitaji na njaa;Huguguna nchi kavu, penye giza la ukiwa na uharibifu.
4. Hung’oa mboga ya chumvi kwenye kichaka;Na mizizi ya mretemu ni chakula chao.
5. Hufukuzwa watoke kati ya watu;Huwapigia kelele kama kumpigia mwivi.
6. Lazima hukaa katika mianya ya mabonde,Katika mashimo ya nchi na ya majabali.
7. Hulia kama punda vichakani;Hukusanyika chini ya upupu.
8. Wao ni wana wa wapumbavu, naam, watoto wa wahuni;Walifukuzwa kwa mijeledi watoke katika nchi.