26. Hapo nilipotazamia mema, ndipo yakaja mabaya;Nami nilipongojea mwanga, likaja giza.
27. Matumbo yangu yatokota, wala hayaachi;Siku za taabu zimenijilia.
28. Naenda nikiomboleza pasipo jua;Nasimama katika mkutano, na kuulilia msaada.
29. Mimi ni ndugu yao mbwa-mwitu,Ni mwenzao mbuni.
30. Ngozi yangu ni nyeusi, nayo yanitoka,Na mifupa yangu imeteketea kwa hari.
31. Kwa hiyo kinanda changu kimegeuzwa kuwa maombolezo,Na filimbi yangu kuwa sauti yao waliao.