Ayu. 30:26-31 Swahili Union Version (SUV)

26. Hapo nilipotazamia mema, ndipo yakaja mabaya;Nami nilipongojea mwanga, likaja giza.

27. Matumbo yangu yatokota, wala hayaachi;Siku za taabu zimenijilia.

28. Naenda nikiomboleza pasipo jua;Nasimama katika mkutano, na kuulilia msaada.

29. Mimi ni ndugu yao mbwa-mwitu,Ni mwenzao mbuni.

30. Ngozi yangu ni nyeusi, nayo yanitoka,Na mifupa yangu imeteketea kwa hari.

31. Kwa hiyo kinanda changu kimegeuzwa kuwa maombolezo,Na filimbi yangu kuwa sauti yao waliao.

Ayu. 30