13. Waiharibu njia yangu,Wauzidisha msiba wangu,Watu wasio na msaidizi.
14. Wanijilia kama wapitao katika ufa mpana;Katikati ya magofu wanishambulia.
15. Vitisho vimenigeukia;Huifukuza heshima yangu kama upepo;Na kufanikiwa kwangu kumepita kama wingu.
16. Sasa nafsi yangu inamwagika ndani yangu;Siku za mateso zimenishika.
17. Wakati wa usiku mifupa yangu huchomeka ndani yangu,Na maumivu yanayonitafuna hayapumziki.
18. Kwa ugonjwa wangu kuwa na nguvu nyingiMavazi yangu yameharibika;Hunikaza kama shingo ya kanzu yangu.
19. Yeye amenibwaga topeni,Nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20. Nakulilia wewe, wala huniitikii;Nasimama, nawe wanitazama tu.
21. Wewe umegeuka kuwa mkali kwangu;Nawe waniudhi kwa uweza wa mkono wako.
22. Waniinua juu hata upeponi, na kunipandisha juu yake;Nawe waniyeyusha katika dhoruba.
23. Kwani najua kuwa utanileta hata kifoni,Niifikilie nyumba waliyoandikiwa wenye uhai wote.
24. Je! Mtu katika kuanguka kwake hanyoshi mkono?Na kulilia msaada katika msiba wake?