Ayu. 30:11-25 Swahili Union Version (SUV)

11. Kwani ameilegeza kamba yake, na kunitesa,Wala hawajizuii tena mbele yangu.

12. Kwa mkono wangu wa kuume huinuka kundi;Huisukuma miguu yangu kando,Na kunipandishia njia zao za uharibifu.

13. Waiharibu njia yangu,Wauzidisha msiba wangu,Watu wasio na msaidizi.

14. Wanijilia kama wapitao katika ufa mpana;Katikati ya magofu wanishambulia.

15. Vitisho vimenigeukia;Huifukuza heshima yangu kama upepo;Na kufanikiwa kwangu kumepita kama wingu.

16. Sasa nafsi yangu inamwagika ndani yangu;Siku za mateso zimenishika.

17. Wakati wa usiku mifupa yangu huchomeka ndani yangu,Na maumivu yanayonitafuna hayapumziki.

18. Kwa ugonjwa wangu kuwa na nguvu nyingiMavazi yangu yameharibika;Hunikaza kama shingo ya kanzu yangu.

19. Yeye amenibwaga topeni,Nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.

20. Nakulilia wewe, wala huniitikii;Nasimama, nawe wanitazama tu.

21. Wewe umegeuka kuwa mkali kwangu;Nawe waniudhi kwa uweza wa mkono wako.

22. Waniinua juu hata upeponi, na kunipandisha juu yake;Nawe waniyeyusha katika dhoruba.

23. Kwani najua kuwa utanileta hata kifoni,Niifikilie nyumba waliyoandikiwa wenye uhai wote.

24. Je! Mtu katika kuanguka kwake hanyoshi mkono?Na kulilia msaada katika msiba wake?

25. Je! Mimi sikulia kwa ajili ya huyo aliyekuwa katika taabu?Nafsi yangu, je! Haikusononeka kwa ajili ya wahitaji?

Ayu. 30