13. Maana hapo ningelala na kutulia;Ningelala usingizi; na kupata kupumzika;
14. Pamoja na wafalme na washauri wa dunia,Hao waliojijengea maganjoni;
15. Au pamoja na wakuu wenye dhahabu,Waliozijaza fedha nyumba zao;
16. Au, kama kuzikwa mimba iliyoharibika, nisingekuwako;Kama wachanga wasiouona mwanga kabisa.
17. Huko waovu huacha kusumbua;Huko nako hao waliochoka wapumzika
18. Huko wafungwa waona raha pamoja;Hawaisikii sauti yake msimamizi.
19. Wakuu na wadogo wako huko;Mtumishi yu huru kwa bwana wake.
20. Mbona yeye aliye mashakani kupewa mwanga,Na hao wenye uchungu rohoni kupewa uhai;