1. Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake.
2. Ayubu akajibu, na kusema;
3. Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi,Na ule usiku uliosema,Mtoto mume ametungishwa mimba.
4. Siku hiyo na iwe giza;Mungu asiiangalie toka juu,Wala mwanga usiiangazie.
5. Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake;Wingu na likae juu yake;Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe.
6. Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu;Usihesabiwe katika siku za mwaka;Wala kutiwa katika hesabu ya miezi.
7. Tazama, usiku huo na uwe tasa;Wala isiwe ndani yake sauti ya shangwe.