Ayu. 28:8-14 Swahili Union Version (SUV)

8. Wanyama wakali wajivunao hawajaikanyaga,Wala simba mkali hajaipita.

9. Huunyoshea mwamba wa gumegume mkono wake;Huipindua milima hata misingi yake.

10. Hukata mifereji kati ya majabali;Na jicho lake huona kila kito cha thamani

11. Hufunga vijito visichuruzike;Na kitu kilichostirika hukifunua.

12. Bali hekima itapatikana wapi?Na mahali pa ufahamu ni wapi?

13. Mwanadamu hajui thamani yake,Wala haionekani katika nchi ya walio hai.

14. Vilindi vyasema, Haimo ndani yangu;Na bahari yasema, Haiko kwangu.

Ayu. 28