8. Wanyama wakali wajivunao hawajaikanyaga,Wala simba mkali hajaipita.
9. Huunyoshea mwamba wa gumegume mkono wake;Huipindua milima hata misingi yake.
10. Hukata mifereji kati ya majabali;Na jicho lake huona kila kito cha thamani
11. Hufunga vijito visichuruzike;Na kitu kilichostirika hukifunua.
12. Bali hekima itapatikana wapi?Na mahali pa ufahamu ni wapi?
13. Mwanadamu hajui thamani yake,Wala haionekani katika nchi ya walio hai.
14. Vilindi vyasema, Haimo ndani yangu;Na bahari yasema, Haiko kwangu.