Ayu. 28:3-14 Swahili Union Version (SUV)

3. Binadamu hukomesha giza;Huyatafuta-tafuta hata mpaka ulio mbali,Mawe ya giza kuu, giza tupu.

4. Hufukua shimo mbali na makao ya watu;Husahauliwa na nyayo zipitazo;Huning’inia mbali na watu, huyumba-yumba huko na huko.

5. Katika ardhi ndimo kitokeamo chakula;Na chini yake hupinduliwa kama kwa moto.

6. Mawe yake ni mahali zipatikanapo yakuti;Nayo ina mchanga wa dhahabu.

7. Njia ile hapana ndege mkali aijuaye,Wala jicho la tai halijaiona;

8. Wanyama wakali wajivunao hawajaikanyaga,Wala simba mkali hajaipita.

9. Huunyoshea mwamba wa gumegume mkono wake;Huipindua milima hata misingi yake.

10. Hukata mifereji kati ya majabali;Na jicho lake huona kila kito cha thamani

11. Hufunga vijito visichuruzike;Na kitu kilichostirika hukifunua.

12. Bali hekima itapatikana wapi?Na mahali pa ufahamu ni wapi?

13. Mwanadamu hajui thamani yake,Wala haionekani katika nchi ya walio hai.

14. Vilindi vyasema, Haimo ndani yangu;Na bahari yasema, Haiko kwangu.

Ayu. 28