3. Binadamu hukomesha giza;Huyatafuta-tafuta hata mpaka ulio mbali,Mawe ya giza kuu, giza tupu.
4. Hufukua shimo mbali na makao ya watu;Husahauliwa na nyayo zipitazo;Huning’inia mbali na watu, huyumba-yumba huko na huko.
5. Katika ardhi ndimo kitokeamo chakula;Na chini yake hupinduliwa kama kwa moto.
6. Mawe yake ni mahali zipatikanapo yakuti;Nayo ina mchanga wa dhahabu.
7. Njia ile hapana ndege mkali aijuaye,Wala jicho la tai halijaiona;
8. Wanyama wakali wajivunao hawajaikanyaga,Wala simba mkali hajaipita.
9. Huunyoshea mwamba wa gumegume mkono wake;Huipindua milima hata misingi yake.
10. Hukata mifereji kati ya majabali;Na jicho lake huona kila kito cha thamani
11. Hufunga vijito visichuruzike;Na kitu kilichostirika hukifunua.
12. Bali hekima itapatikana wapi?Na mahali pa ufahamu ni wapi?
13. Mwanadamu hajui thamani yake,Wala haionekani katika nchi ya walio hai.
14. Vilindi vyasema, Haimo ndani yangu;Na bahari yasema, Haiko kwangu.