Ayu. 28:13-16 Swahili Union Version (SUV)

13. Mwanadamu hajui thamani yake,Wala haionekani katika nchi ya walio hai.

14. Vilindi vyasema, Haimo ndani yangu;Na bahari yasema, Haiko kwangu.

15. Haipatikani kwa dhahabu,Wala fedha haitapimwa iwe thamani yake.

16. Haiwezi kutiwa thamani kwa dhahabu ya Ofiri,Wala kwa shohamu ya thamani nyingi, wala kwa yakuti ya samawi.

Ayu. 28