1. Hakika kuna shimo wachimbako fedha,Na mahali wapatapo dhahabu waisafishayo.
2. Chuma hufukuliwa katika ardhi,Na shaba huyeyushwa katika mawe.
3. Binadamu hukomesha giza;Huyatafuta-tafuta hata mpaka ulio mbali,Mawe ya giza kuu, giza tupu.
4. Hufukua shimo mbali na makao ya watu;Husahauliwa na nyayo zipitazo;Huning’inia mbali na watu, huyumba-yumba huko na huko.
5. Katika ardhi ndimo kitokeamo chakula;Na chini yake hupinduliwa kama kwa moto.
6. Mawe yake ni mahali zipatikanapo yakuti;Nayo ina mchanga wa dhahabu.