7. Hujilaza usiku kucha uchi pasipo nguo,Wala hawana cha kujifunika baridi.
8. Hutota kwa manyunyo ya milimani,Na kuambatana na jabali kwa kukosa sitara,
9. Wako wamwondoao matitini kwa nguvu huyo asiye na baba,Na kutwaa rehani kwa maskini;
10. Hata wazunguke uchi pasipo mavazi,Nao wakiwa na njaa huchukua miganda;
11. Hushindika mafuta ndani ya makuta ya watu hao;Wakanyaga mashinikizo, nao wana kiu.
12. Watu huugua toka mji ulio na watu wengi,Na roho yake aliyejeruhiwa hupiga ukelele;Wala Mungu hauangalii upumbavu.
13. Hawa ni katika hao waliouasi mwanga;Hawazijui njia zake,Wala hawakai katika mapito yake.
14. Mwuaji huamka asubuhi kukipambauka, huwaua maskini na wahitaji;Tena wakati wa usiku yu kama mwivi.
15. Tena jicho lake mzinifu hungojea wakati wa giza-giza,Akisema, Hapana jicho litakaloniona;Naye huuficha uso wake.
16. Wao hutoboa nyumba gizani;Hujifungia ndani wakati wa mchana;Hawaujui mwanga.
17. Kwani asubuhi kwao wote ni kama giza tupu;Kwani wao wavijua vitisho vya hiyo giza tupu.
18. Mwasema, Yeye ni mwepesi juu ya uso wa gharika;Sehemu yao inalaaniwa duniani;Hageuki kwenda njia ya mizabibuni.
19. Chaka na hari hukausha maji ya theluji;Kuzimu nako hao ambao wamefanya dhambi.
20. Tumbo lililomzaa litamsahau; buu litamla na kuona tamu;Hatakumbukwa tena;Na udhalimu utavunjwa kama mti.
21. Naam, yeye huwala walio tasa wasiozaa;Wala hamtendei mema mwanamke mjane.
22. Lakini Mungu huwadumisha wenye uwezo kwa nguvu zake;Huinuka, wasiokuwa na tumaini la kuishi.
23. Huwapa kuwa na salama, nao wapumzika kwayo;Na macho yake ya juu ya njia zao.
24. Wao wametukuzwa; lakini kitambo kidogo hutoweka;Naam, hushushwa, na kuondolewa njiani kama wengine wote,Nao hukatwa kama vile masuke ya ngano.
25. Na kama sivyo sasa, ni nani atakayenihukumu kuwa ni mwongo,Na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?