6. Hukata nafaka zao mashambani;Na kuokota zabibu za waovu.
7. Hujilaza usiku kucha uchi pasipo nguo,Wala hawana cha kujifunika baridi.
8. Hutota kwa manyunyo ya milimani,Na kuambatana na jabali kwa kukosa sitara,
9. Wako wamwondoao matitini kwa nguvu huyo asiye na baba,Na kutwaa rehani kwa maskini;
10. Hata wazunguke uchi pasipo mavazi,Nao wakiwa na njaa huchukua miganda;
11. Hushindika mafuta ndani ya makuta ya watu hao;Wakanyaga mashinikizo, nao wana kiu.
12. Watu huugua toka mji ulio na watu wengi,Na roho yake aliyejeruhiwa hupiga ukelele;Wala Mungu hauangalii upumbavu.
13. Hawa ni katika hao waliouasi mwanga;Hawazijui njia zake,Wala hawakai katika mapito yake.
14. Mwuaji huamka asubuhi kukipambauka, huwaua maskini na wahitaji;Tena wakati wa usiku yu kama mwivi.
15. Tena jicho lake mzinifu hungojea wakati wa giza-giza,Akisema, Hapana jicho litakaloniona;Naye huuficha uso wake.
16. Wao hutoboa nyumba gizani;Hujifungia ndani wakati wa mchana;Hawaujui mwanga.
17. Kwani asubuhi kwao wote ni kama giza tupu;Kwani wao wavijua vitisho vya hiyo giza tupu.
18. Mwasema, Yeye ni mwepesi juu ya uso wa gharika;Sehemu yao inalaaniwa duniani;Hageuki kwenda njia ya mizabibuni.