5. Tazama, kama punda-mwitu jangwaniWao hutoka kwenda kazini mwao, wakitafuta chakula kwa bidii;Jangwa huwapa chakula cha watoto wao.
6. Hukata nafaka zao mashambani;Na kuokota zabibu za waovu.
7. Hujilaza usiku kucha uchi pasipo nguo,Wala hawana cha kujifunika baridi.
8. Hutota kwa manyunyo ya milimani,Na kuambatana na jabali kwa kukosa sitara,