20. Tumbo lililomzaa litamsahau; buu litamla na kuona tamu;Hatakumbukwa tena;Na udhalimu utavunjwa kama mti.
21. Naam, yeye huwala walio tasa wasiozaa;Wala hamtendei mema mwanamke mjane.
22. Lakini Mungu huwadumisha wenye uwezo kwa nguvu zake;Huinuka, wasiokuwa na tumaini la kuishi.
23. Huwapa kuwa na salama, nao wapumzika kwayo;Na macho yake ya juu ya njia zao.
24. Wao wametukuzwa; lakini kitambo kidogo hutoweka;Naam, hushushwa, na kuondolewa njiani kama wengine wote,Nao hukatwa kama vile masuke ya ngano.
25. Na kama sivyo sasa, ni nani atakayenihukumu kuwa ni mwongo,Na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?