Ayu. 24:20-25 Swahili Union Version (SUV)

20. Tumbo lililomzaa litamsahau; buu litamla na kuona tamu;Hatakumbukwa tena;Na udhalimu utavunjwa kama mti.

21. Naam, yeye huwala walio tasa wasiozaa;Wala hamtendei mema mwanamke mjane.

22. Lakini Mungu huwadumisha wenye uwezo kwa nguvu zake;Huinuka, wasiokuwa na tumaini la kuishi.

23. Huwapa kuwa na salama, nao wapumzika kwayo;Na macho yake ya juu ya njia zao.

24. Wao wametukuzwa; lakini kitambo kidogo hutoweka;Naam, hushushwa, na kuondolewa njiani kama wengine wote,Nao hukatwa kama vile masuke ya ngano.

25. Na kama sivyo sasa, ni nani atakayenihukumu kuwa ni mwongo,Na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?

Ayu. 24