18. Mwasema, Yeye ni mwepesi juu ya uso wa gharika;Sehemu yao inalaaniwa duniani;Hageuki kwenda njia ya mizabibuni.
19. Chaka na hari hukausha maji ya theluji;Kuzimu nako hao ambao wamefanya dhambi.
20. Tumbo lililomzaa litamsahau; buu litamla na kuona tamu;Hatakumbukwa tena;Na udhalimu utavunjwa kama mti.
21. Naam, yeye huwala walio tasa wasiozaa;Wala hamtendei mema mwanamke mjane.
22. Lakini Mungu huwadumisha wenye uwezo kwa nguvu zake;Huinuka, wasiokuwa na tumaini la kuishi.