12. Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake;Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu,
13. Lakini yeye ni mmoja, ni nani awezaye kumgeuza?Tena nafsi yake ilitakalo, ndilo afanyalo.
14. Kwani yeye hulitimiliza hilo nililoamuriwa;Tena mambo mengi kama hayo ya pamoja naye.
15. Kwa hiyo naona taabu mbele ya uso wake;Nitakapofikiri, namwogopa.
16. Kwani Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia,Naye Mwenyezi amenitaabisha;
17. Maana sikufadhaishwa kwa sababu ya giza,Wala kwa sababu giza kuu limenifunika uso.