7. Hukumpa maji ya kunywa huyo aliyechoka,Nawe umemnyima chakula huyo mwenye njaa.
8. Lakini huyo shujaa, nchi ilikuwa yake;Na huyo mwenye kusifiwa, yeye aliikaa.
9. Umewafukuza wanawake wajane hali ya utupu,Na mikono ya mayatima imevunjwa.
10. Kwa hiyo umezungukwa na mitego,Na hofu ya ghafula yakutaabisha,
11. Au je! Huoni giza,Na maji mengi yanayokufunika?
12. Je! Mungu hayuko mbinguni juu?Tena tazama umbali wa nyota, jinsi zilivyo juu!
13. Nawe wasema, Mungu anajua nini?Je! Aweza kuamua kati ya giza kuu?
14. Mawingu mazito ni kifuniko chake, hata asione;Naye yuatembea juu ya kuba ya mbingu.