Ayu. 22:25-30 Swahili Union Version (SUV)

25. Naye Mwenyezi atakuwa hazina yako,Atakuwa ni fedha ya thamani kwako.

26. Kwani ndipo utakapojifurahisha katika Mwenyezi,Na kuinua uso wako kumwelekea Mungu.

27. Utamwomba yeye naye atakusikia;Nawe utazitimiliza nadhiri zako.

28. Nawe utakusudia neno, nalo litathibitika kwako;Na mwanga utaziangazia njia zako.

29. Hapo watakapokuangusha, utasema, Kuna kuinuka tena;Naye mnyenyekevu Mungu atamwokoa.

30. Atamwokoa na huyo asiye na hatia;Naam, utaokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.

Ayu. 22