24. Nawe hazina zako ziweke mchangani,Na dhahabu ya Ofiri iweke kati ya mawe ya vijito;
25. Naye Mwenyezi atakuwa hazina yako,Atakuwa ni fedha ya thamani kwako.
26. Kwani ndipo utakapojifurahisha katika Mwenyezi,Na kuinua uso wako kumwelekea Mungu.
27. Utamwomba yeye naye atakusikia;Nawe utazitimiliza nadhiri zako.
28. Nawe utakusudia neno, nalo litathibitika kwako;Na mwanga utaziangazia njia zako.
29. Hapo watakapokuangusha, utasema, Kuna kuinuka tena;Naye mnyenyekevu Mungu atamwokoa.
30. Atamwokoa na huyo asiye na hatia;Naam, utaokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.