Ayu. 22:15-19 Swahili Union Version (SUV)

15. Je! Utaiandama njia ya zamaniWaliyoikanyaga watu waovu?

16. Ambao walinyakuliwa kabla ya wakati wao,Msingi wao ulimwagika kama kijito cha maji;

17. Waliomwambia Mungu, Tuondokee;Tena, Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?

18. Naye ndiye aliyezijaza nyumba zao vitu vyema;Lakini mashauri ya waovu na yawe mbali nami.

19. Wenye haki huyaona hayo wakafurahi;Nao wasio na hatia huwacheka;

Ayu. 22