Ayu. 22:13-30 Swahili Union Version (SUV)

13. Nawe wasema, Mungu anajua nini?Je! Aweza kuamua kati ya giza kuu?

14. Mawingu mazito ni kifuniko chake, hata asione;Naye yuatembea juu ya kuba ya mbingu.

15. Je! Utaiandama njia ya zamaniWaliyoikanyaga watu waovu?

16. Ambao walinyakuliwa kabla ya wakati wao,Msingi wao ulimwagika kama kijito cha maji;

17. Waliomwambia Mungu, Tuondokee;Tena, Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?

18. Naye ndiye aliyezijaza nyumba zao vitu vyema;Lakini mashauri ya waovu na yawe mbali nami.

19. Wenye haki huyaona hayo wakafurahi;Nao wasio na hatia huwacheka;

20. Wasema, Hakika hao waliotuinukia wamekatiliwa mbali,Na mabaki yao moto umeyateketeza.

21. Mjue sana Mungu, ili uwe na amani;Ndivyo mema yatakavyokujia.

22. Uyapokee, tafadhali, mafunzo yatokayo kinywani mwake,Na maneno yake yaweke moyoni mwako.

23. Ukimrudia Mwenyezi, utajengwa;Ukiuondoa udhalimu mbali na hema yako.

24. Nawe hazina zako ziweke mchangani,Na dhahabu ya Ofiri iweke kati ya mawe ya vijito;

25. Naye Mwenyezi atakuwa hazina yako,Atakuwa ni fedha ya thamani kwako.

26. Kwani ndipo utakapojifurahisha katika Mwenyezi,Na kuinua uso wako kumwelekea Mungu.

27. Utamwomba yeye naye atakusikia;Nawe utazitimiliza nadhiri zako.

28. Nawe utakusudia neno, nalo litathibitika kwako;Na mwanga utaziangazia njia zako.

29. Hapo watakapokuangusha, utasema, Kuna kuinuka tena;Naye mnyenyekevu Mungu atamwokoa.

30. Atamwokoa na huyo asiye na hatia;Naam, utaokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.

Ayu. 22