12. Je! Mungu hayuko mbinguni juu?Tena tazama umbali wa nyota, jinsi zilivyo juu!
13. Nawe wasema, Mungu anajua nini?Je! Aweza kuamua kati ya giza kuu?
14. Mawingu mazito ni kifuniko chake, hata asione;Naye yuatembea juu ya kuba ya mbingu.
15. Je! Utaiandama njia ya zamaniWaliyoikanyaga watu waovu?
16. Ambao walinyakuliwa kabla ya wakati wao,Msingi wao ulimwagika kama kijito cha maji;
17. Waliomwambia Mungu, Tuondokee;Tena, Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?
18. Naye ndiye aliyezijaza nyumba zao vitu vyema;Lakini mashauri ya waovu na yawe mbali nami.
19. Wenye haki huyaona hayo wakafurahi;Nao wasio na hatia huwacheka;
20. Wasema, Hakika hao waliotuinukia wamekatiliwa mbali,Na mabaki yao moto umeyateketeza.
21. Mjue sana Mungu, ili uwe na amani;Ndivyo mema yatakavyokujia.