Ayu. 21:26-30 Swahili Union Version (SUV)

26. Wao hulala mavumbini sawasawa,Mabuu huwafunika.

27. Tazama, nayajua mawazo yenu,Na mashauri mnayoazimia kwa uovu juu yangu.

28. Kwa kuwa mwasema, Nyumba ya huyo mkuu i wapi?Na hema waliyoikaa hao waovu i wapi?

29. Je! Hamkuwauliza wapitao njiani?Na maonyo yao hamyajui?

30. Kwamba mwovu huachiliwa katika siku ya msiba?Na kuongozwa nje katika siku ya ghadhabu?

Ayu. 21