22. Je! Mtu awaye yote atamfundisha Mungu maarifa?Naye ndiye awahukumuye walioko juu.
23. Mmoja hufa katika nguvu zake kamili,Mwenye kukaa salama na kustarehe;
24. Vyombo vyake vimejaa maziwa,Na mafuta ya mifupani mwake ni laini.
25. Mwingine hufa katika uchungu wa roho,Asionje mema kamwe.
26. Wao hulala mavumbini sawasawa,Mabuu huwafunika.
27. Tazama, nayajua mawazo yenu,Na mashauri mnayoazimia kwa uovu juu yangu.
28. Kwa kuwa mwasema, Nyumba ya huyo mkuu i wapi?Na hema waliyoikaa hao waovu i wapi?
29. Je! Hamkuwauliza wapitao njiani?Na maonyo yao hamyajui?
30. Kwamba mwovu huachiliwa katika siku ya msiba?Na kuongozwa nje katika siku ya ghadhabu?
31. Ni nani atakayetangaza njia yake usoni pake?Tena ni nani atakayemlipa kwa hayo aliyofanya?
32. Pamoja na hayo atachukuliwa kaburini,Nao watalinda zamu juu ya ziara lake.