Ayu. 20:9-16 Swahili Union Version (SUV)

9. Jicho lililomwona halitamwona tena;Wala mahali pake hapatamtazama tena.

10. Watoto wake watataka fadhili kwa maskini,Na mikono yake itarudisha mali yake.

11. Mifupa yake imejaa ujana wake,Lakini utalala nchi naye mavumbini.

12. Ingawa uovu una tamu kinywani mwake,Ingawa auficha chini ya ulimi wake;

13. Ingawa auhurumia, asikubali kuuacha uende zake.Lakini akaushika vivyo kinywani mwake;

14. Hata hivyo chakula chake matumboni mwake kinabadilika,Kimekuwa ni nyongo za majoka ndani yake.

15. Amemeza mali, naye atayatapika tena;Mungu atayatoa tumboni mwake.

16. Ataamwa sumu ya majoka;Na ulimi wa fira utamwua.

Ayu. 20