4. Je! Hujui neno hili tangu zamani za kale,Tangu wanadamu kuwekwa juu ya nchi,
5. Ya kuwa shangwe ya waovu ni kwa muda kidogo,Na furaha ya wapotovu ni ya dakika moja tu?
6. Ujapopanda ukuu wake mpaka mbinguni,Na kichwa chake kufikilia mawinguni;
7. Hata hivyo ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe;Hao waliomwona watasema, Yuko wapi?
8. Ataruka mfano wa ndoto, asionekane;Naam, atafukuzwa kama maono ya usiku,
9. Jicho lililomwona halitamwona tena;Wala mahali pake hapatamtazama tena.
10. Watoto wake watataka fadhili kwa maskini,Na mikono yake itarudisha mali yake.
11. Mifupa yake imejaa ujana wake,Lakini utalala nchi naye mavumbini.
12. Ingawa uovu una tamu kinywani mwake,Ingawa auficha chini ya ulimi wake;
13. Ingawa auhurumia, asikubali kuuacha uende zake.Lakini akaushika vivyo kinywani mwake;