18. Aliyoyataabikia kazi atayarudisha, asiyameze;Kwa mali aliyoyapata, hatafurahi.
19. Kwa maana amewaonea na kuwaacha maskini;Amenyang’anya nyumba kwa jeuri, wala hataijenga.
20. Kwa sababu hakujua utulivu ndani yake,Hataponya cho chote katika hicho alichokifurahia.
21. Hakikusalia kitu asichokula;Kwa hiyo kufanikiwa kwake hakutadumu.
22. Katika kujaa kwa wingi wake atakuwa katika dhiki;Mkono wa kila anayesumbuliwa utamjia.
23. Hapo atakapo kulijaza tumbo lake,Mungu atamtupia ukali wa ghadhabu zake,Na kuunyesha juu yake akiwa anakula.
24. Ataikimbia silaha ya chuma,Na uta wa shaba utamchoma kwa pili.