Ayu. 20:15-22 Swahili Union Version (SUV)

15. Amemeza mali, naye atayatapika tena;Mungu atayatoa tumboni mwake.

16. Ataamwa sumu ya majoka;Na ulimi wa fira utamwua.

17. Hataiangalia hiyo mito ya maji,Vile vijito vilivyojaa asali na siagi.

18. Aliyoyataabikia kazi atayarudisha, asiyameze;Kwa mali aliyoyapata, hatafurahi.

19. Kwa maana amewaonea na kuwaacha maskini;Amenyang’anya nyumba kwa jeuri, wala hataijenga.

20. Kwa sababu hakujua utulivu ndani yake,Hataponya cho chote katika hicho alichokifurahia.

21. Hakikusalia kitu asichokula;Kwa hiyo kufanikiwa kwake hakutadumu.

22. Katika kujaa kwa wingi wake atakuwa katika dhiki;Mkono wa kila anayesumbuliwa utamjia.

Ayu. 20