13. Ingawa auhurumia, asikubali kuuacha uende zake.Lakini akaushika vivyo kinywani mwake;
14. Hata hivyo chakula chake matumboni mwake kinabadilika,Kimekuwa ni nyongo za majoka ndani yake.
15. Amemeza mali, naye atayatapika tena;Mungu atayatoa tumboni mwake.
16. Ataamwa sumu ya majoka;Na ulimi wa fira utamwua.
17. Hataiangalia hiyo mito ya maji,Vile vijito vilivyojaa asali na siagi.
18. Aliyoyataabikia kazi atayarudisha, asiyameze;Kwa mali aliyoyapata, hatafurahi.
19. Kwa maana amewaonea na kuwaacha maskini;Amenyang’anya nyumba kwa jeuri, wala hataijenga.
20. Kwa sababu hakujua utulivu ndani yake,Hataponya cho chote katika hicho alichokifurahia.
21. Hakikusalia kitu asichokula;Kwa hiyo kufanikiwa kwake hakutadumu.