Ayu. 20:13-21 Swahili Union Version (SUV)

13. Ingawa auhurumia, asikubali kuuacha uende zake.Lakini akaushika vivyo kinywani mwake;

14. Hata hivyo chakula chake matumboni mwake kinabadilika,Kimekuwa ni nyongo za majoka ndani yake.

15. Amemeza mali, naye atayatapika tena;Mungu atayatoa tumboni mwake.

16. Ataamwa sumu ya majoka;Na ulimi wa fira utamwua.

17. Hataiangalia hiyo mito ya maji,Vile vijito vilivyojaa asali na siagi.

18. Aliyoyataabikia kazi atayarudisha, asiyameze;Kwa mali aliyoyapata, hatafurahi.

19. Kwa maana amewaonea na kuwaacha maskini;Amenyang’anya nyumba kwa jeuri, wala hataijenga.

20. Kwa sababu hakujua utulivu ndani yake,Hataponya cho chote katika hicho alichokifurahia.

21. Hakikusalia kitu asichokula;Kwa hiyo kufanikiwa kwake hakutadumu.

Ayu. 20