7. Tazama, nalia, Udhalimu, lakini sisikiwi;Naulilia msaada, wala hapana hukumu.
8. Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita,Na kutia giza katika mapito yangu.
9. Amenivua utukufu wangu,Na kuiondoa taji kichwani mwangu.
10. Amenibomoa pande zote, nami nimetoweka;Na tumaini langu ameling’oa kama mti.
11. Tena ameziwasha ghadhabu zake juu yangu,Akanihesabia kuwa mmoja katika watesi wake.
12. Majeshi yake husongea pamoja, na kunipandishia njia yao,Na kupiga marago kuizunguka hema yangu.
13. Amewaweka ndugu zangu mbali nami,Na wanijuao wametengwa nami kabisa.
14. Watu wa mbari yangu wamekoma,Na rafiki zangu niwapendao wamenisahau.
15. Wakaao nyumbani mwangu, na vijakazi vyangu, wanihesabu kuwa mgeni;Mimi ni mgeni machoni pao.
16. Namwita mtumishi wangu, wala haniitikii,Ingawa namsihi kwa kinywa changu.