1. Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2. Je! Mtanichukiza nafsi yangu hata lini,Na kunivunja-vunja kwa maneno?
3. Mara kumi hizi mmenishutumu;Hamwoni haya kunifanyia mambo magumu.
4. Ingawaje nimekosa,Kosa langu hukaa kwangu mwenyewe.
5. Kwamba mtajitukuza juu yangu,Na kunena juu yangu shutumu langu;
6. Jueni basi kuwa Mungu amenipotosha,Na kunizingira kwa wavu wake.
7. Tazama, nalia, Udhalimu, lakini sisikiwi;Naulilia msaada, wala hapana hukumu.
8. Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita,Na kutia giza katika mapito yangu.