Ayu. 19:1-8 Swahili Union Version (SUV)

1. Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,

2. Je! Mtanichukiza nafsi yangu hata lini,Na kunivunja-vunja kwa maneno?

3. Mara kumi hizi mmenishutumu;Hamwoni haya kunifanyia mambo magumu.

4. Ingawaje nimekosa,Kosa langu hukaa kwangu mwenyewe.

5. Kwamba mtajitukuza juu yangu,Na kunena juu yangu shutumu langu;

6. Jueni basi kuwa Mungu amenipotosha,Na kunizingira kwa wavu wake.

7. Tazama, nalia, Udhalimu, lakini sisikiwi;Naulilia msaada, wala hapana hukumu.

8. Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita,Na kutia giza katika mapito yangu.

Ayu. 19