Ayu. 17:8-16 Swahili Union Version (SUV)

8. Walekevu watayastaajabia hayo,Na asiye na hatia atajiamsha juu ya mpotovu.

9. Lakini mwenye haki ataishika njia yake,Naye mwenye mikono safi atazidi kupata nguvu.

10. Lakini rudini; ninyi nyote, njoni sasa;Wala sitampata mtu mwenye hekima kati yenu.

11. Siku zangu zimepita, makusudi yangu yamevunjika,Hata hayo niliyo nayo moyoni mwangu.

12. Wabadili usiku kuwa mchana;Wasema, Mwanga u karibu kwa sababu ya giza.

13. Nikitazamia kuzimu kuwa nyumba yangu;Nikitandika malazi yangu gizani;

14. Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu;Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na umbu langu;

15. Basi, tumaini langu li wapi?Na tumaini langu, ni nani atakayeliona?

16. Litashuka kwenye makomeo ya kuzimu,Itakapokuwapo raha mavumbini.

Ayu. 17