Ayu. 17:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Roho yangu imezimika, siku zangu zimekoma,Kaburi i tayari kunipokea.

2. Ni kweli wako kwangu wenye kufanya dhihaka,Jicho langu hukaa katika kunifanyia uchungu kwao.

3. Nipe rehani basi, uwe dhamana kwa ajili yangu kwako wewe mwenyewe;Kuna nani atakayeniwekea dhamana?

4. Kwani mioyo yao imeificha ufahamu;Kwa hiyo hutawakuza.

5. Awafitiniye rafiki zake wawe mawindo,Hata macho ya watoto wake yataingia kiwi.

6. Amenifanya niwe simo kwa watu;Nimekuwa mwenye kuchukiwa kwa wazi.

Ayu. 17