5. Kwani uovu wako unakufundisha kinywa chako,Nawe wachagua ulimi wake mwenye hila.
6. Kinywa chako mwenyewe chakuhukumia makosa, wala si mimi;Naam, midomo yako mwenyewe hushuhudia juu yako.
7. Je! Wewe u mtu wa kwanza aliyezaliwa?Au, ulizawa wewe kabla ya milima?
8. Je! Umesikia mashauri ya siri ya Mungu?Nawe je! Wazuia hekima iwe yako tu?
9. Je! Wewe wajua neno lipi, ambalo sisi hatulijui?Nawe wafahamu nini, ambalo halimo ndani yetu?