Ayu. 15:30-33 Swahili Union Version (SUV)

30. Hataondoka gizani;Ndimi za moto zitayakausha matawi yake,Naye ataondoka kwa pumzi za kinywa chake.

31. Asiutumainie ubatili, na kujidanganya;Kwa kuwa huo ubatili ndio utakaokuwa ujira wake.

32. Jambo hili litatendeka kabla ya wakati wake,Na tawi lake halitasitawi.

33. Atayapukutisha mapooza yake kama mzabibu,Na kuyatupa maua yake kama mzeituni.

Ayu. 15