30. Hataondoka gizani;Ndimi za moto zitayakausha matawi yake,Naye ataondoka kwa pumzi za kinywa chake.
31. Asiutumainie ubatili, na kujidanganya;Kwa kuwa huo ubatili ndio utakaokuwa ujira wake.
32. Jambo hili litatendeka kabla ya wakati wake,Na tawi lake halitasitawi.
33. Atayapukutisha mapooza yake kama mzabibu,Na kuyatupa maua yake kama mzeituni.