16. Sembuse mtu ambaye ni mwenye kuchukiza na uchafu,Mwanadamu anywaye uovu kama anywavyo maji!
17. Mimi nitakuonyesha, unisikilize;Na hayo yote niliyoyaona nitayanena;
18. (Ambayo watu wenye hekima wameyatangazaTokea baba zao, wala hawakuyaficha;
19. Waliopewa hiyo nchi peke yao,Wala mgeni hakupita kati yao);
20. Mtu mwovu huwa na uchungu siku zake zote,Hata hesabu ya miaka aliyowekewa mwenye kuonea.
21. Sauti za utisho zi masikioni mwake;Katika kufanikiwa kwake mtekaji nyara atamjia juu yake;
22. Yeye hasadiki kwamba atarudi kutoka gizani,Naye hungojewa na upanga;
23. Hutanga-tanga ili apate chakula, akisema, Ki wapi?Ajua kwamba siku ya giza i tayari karibu yake;
24. Mateso na dhiki humtia hofu;Humshinda kama vile mfalme aliye tayari kwa vita;
25. Kwa kuwa amenyosha mkono wake juu ya Mungu,Na kuendelea kwa kiburi kinyume cha Mwenyezi;
26. Humshambulia na shingo ngumu,Kwa mafundo makubwa ya ngao zake;
27. Kwa kuwa amefunika uso wake na kunona kwake,Na kuwandisha mafuta kiunoni mwake;Naye amekaa katika miji iliyo ukiwa,
28. Katika nyumba ambazo hapana mtu azikaaye,Zilizokuwa tayari kuwa magofu.
29. Hatakuwa tajiri, wala mali zake hazitadumu,Wala maongeo yao hayatainama nchi.
30. Hataondoka gizani;Ndimi za moto zitayakausha matawi yake,Naye ataondoka kwa pumzi za kinywa chake.
31. Asiutumainie ubatili, na kujidanganya;Kwa kuwa huo ubatili ndio utakaokuwa ujira wake.
32. Jambo hili litatendeka kabla ya wakati wake,Na tawi lake halitasitawi.